Friday, February 15, 2008

Dada yetu wa kichina

Dada yetu, "Hoang Hwe", wa Beijing China akirusha teke nyoofu la pembeni (yop chaggi) "Masela" kuweni makini..Mungu akitujalia atakuja bongo mwaka huu. Lakini..psssstt...chonde chonde..nanihii..eehh..mmhh msi..msih..msije mkajaribu kumpora kisimu chake..Nomaaa..Aibuu...

Civilian Anti - Terrorist and Tactical Self Defense. (Practical Combat Application)

The Talons of the Eagle. The gangster is trying to...Anyway..you know..Like lightning you go for his throat using the Eagle's Talons. Go in hard and fast..Has your "self defense master" ever taught you stuff like this? The answer is in your heart.

You think this is a gangster movie..right? (Note the point where the eagle's talons are pressing) You hold the point, press, twist and pull...vigorously. This is a single movement. At the same time you transfer your Ki (Chi or Qi) from the point, 2 inches, just below your navel to his respective meridian points on the side of his throat. Game over!! That will most likely be his last attempt..

Sonkal Yop Terigi (knife hand strike) at the would be assailant's throat is a "total stopper" Precisely done..and you will have to decide where to dump him..at a Police station, a hospital or anywhere convenient? You choose..he goes..

Throwing a punch in a small and confined area (in this case a car). If your Sabum, Sensei, Sifu, Guru or Masta doesn't teach & train you how to do such things and he is telling you that hii ndio staili kiboko..hakugusi mtu..He is lying to you!! That's it. You do the above move, i.e. hitting the punch pad, 300 times per side. All hits must be precise and powerful.

1st Dan Graduation

1st Degree (Dan) Black Belt Graduation..way back in 1996. "Lady Bouncer" (front row, seated, fourth from left) Are you still in the "Game?". The black belts are sitting on the right & left hand side of Sabum Sin Jae Sop (7th Dan) and his wife Sabum Madam Cha Son Yong ( 6th Dan). 18 went in, only 4 came out with black belts...Duuh..Aiseeh..

TKD COMMONWEALTH DAY DEMO

Commonwealth Day Taekwon-do Demonstration in progress. Superbly performed by Shaaban Robert Secondary School Tkd Team.

Shabrob Sec Shool Tkd Team

Shaaban Robert Tkd Demo Team..Warming up before the Commonwealth Day Celebrations.

Contemplatation....

Shaaban Robert Secondary School Taekwon-do Trainee in deep mawazo...Mungu wangu!! Just after baptism by 200 squat jumps..up the stairs

Tuesday, February 12, 2008

Kong-Soo Do

Watu wengi hufikiri kuwa Taekwon-do ni Karate ya Korea. Hii si sahihi.

Karate ya Korea inaitwa Kong Soo.

Kong-Soo Do

Historia ya sanaa hii na nyingine nyingi za Korea tunaweza kuigawa sehemu mbili;

(i) Kabla ya Uvamizi wa Wajapani { - 1910}

(ii) Baada ya Uvamizi au Wakati wa Utawala wa kikoloni wa Kijapani.

Hapa tutazungumzia (ii) zama za 1910 hadi leo.

Mnamo mwaka 1910, Majeshi ya Kijapani yalilivamia taifa la Korea na kulifanya kuwa koloni lake.
Ili kuhakikisha ya kuwa wanautokomeza utamaduni wa Kikorea wakoloni wa kijapani walifanya mambo matatu;

(i) Waliharibu na kuchoma kumbukumbu zote za kihistoria za wakorea ikiwa ni pamoja na maandiko ya mapokeo yao ya kihistoria ambayo yalijumuisha historia ya sanaa za mapigano.

(ii) Walizuia na kupiga marufuku wakorea kujifunza sanaa zao za asili ikiwa ni pamoja na zile za mapigano.

(iii) Walibadilisha mfumo wa elimu na kulazimisha mfumo wa elimu wa kijapani ndio utumike korea. Hii ni elimu kuanzia msingi, sekondari na kuendelea.

Lengo lao kuu ni kuweza kutawala kwa urahisi kwani walikuwa na imani kuwa binadamu asiye na kumbukumbu za kihistoria au asiye na utamaduni wake wa asili ni rahisi kutawaliwa.

Kilichotokea ni kwamba idadi kubwa ya vijana wa kikorea walipelekwa japani kwenda kupata elimu ya sekondati na vyuo vya juu. Huko (japani) mbali na elimu ya kawaida pia walijifunza sanaa zakijapani za mapambano ya mikono mitupu ikiwa ni pamoja na karate, jiu-jitsu, judo, kendo nakadhalika.

Mnamo mwaka 1945 wakati wa kilele cha vita kuu ya pili ya dunia, Japan ilisalimu amri kwa Marekani na washirika wake. Tukio hili pia lilimaanisha kuwa utawala wa kikoloni wa Japan huko Korea ulifika ukingoni na hivyo basi Korea ikawa ni nchi huru.

Uhuru huu ni pamoja na kuwa huru kufanya yale yote ambayo hapo awali wakoloni wakijapani waliyakataza.

Tatizo; wapi pakuanzia wakati hamna kumbukumbu?

Jambo la heri lililokuwa limetokea ni kwamba wakoloni hawakuwazuia shughuli ndogo za kitamaduni na kidini kwahiyo baadhi ya wakorea waliweza kuendelea kujifunza sanaa za mapambano ya mikono mitupu chini ya kivuli cha ngoma za asili au ibada katika mahekalu. Sanaa zilizofichwa kwa namna hii ni Tae Kyon na Soo Bakh Ki au Soo Bakh Do.

Kwahiyo utaona kwamba kuna vijana wa Korea walienda Japan kwa ajili ya masomo wakiwa tayari na ujuzi fulani wa sanaa hizi za mapigano. Pamoja na masomo yao na shughuli nyingine pia walijifunza sanaa za kijapani za mapigano.

Baada ya uhuru wakorea hao wakarudi nyumbani (Korea). Huko wakafungua shule (ninaposema shule namaanisha shule za sanaa za mapigano) na katika kujitangaza na kwa kuwa kulikuwa bado hamna sanaa za mapigano za Korea zilizokuwa hadharani wengi wakaziita sanaa zao Kong – Soo Do.

Kong-Soo Do ni tafsiri ya neno Karate-Do katika lugha ya Korea. Yaani; yale maandishi ya kijapani ambayo husomeka Karate-Do kwa kikorea tafsiri ya neno hilo linatamkwa “Kong-Soo Do”.

Mitindo (Style) mingi ya Kong-Soo (Karate) ilianza kufundishwa, mojawapo ya mitindo hiyo ni “Song Moo Kwan”.

Song Moo Kwan ni matamko ya kikorea ya neno Shotokan.

Tanzania kuna mitindo mbalimbali ya Karate, ila yenye wafuasi wengi ni Shotokan na Goju-ryu.

Muasisi wa “Song Moo Kwan” anaitwa Byung Rick Ro. Huyu alizaliwa tarehe 3 Julai, 1919 huko Kaesung, Korea. Akiwa mtoto, umri wa miaka yapata 12 hivi alianza kuhudhuria mafunzo ya sanaa zilizokuwa zinafundishwa kwa kificho chini ya mwamvuli wa ibada kwenye hekalu lililokuwa jirani na nyumbani kwao. Sanaa alizojifunza zilikuwa Soo Bakh Kin na Tae Kyon. Alipotimiza miaka 17 alikwenda Japan kwa ajili ya masomo. Huku akiendelea na masomo kwenye chuo kilichokuwa kinaitwa Chou, alianza pia kujifunza Shotokan Karate chini ya muasisi wa sanaa hiyo, Gichin Funakoshi.

Mnamo tarehe 2 Mei, 1946, Byung Rick Ro alifungua rasmi shule na kuuita mtindo aliokuwa anafundisha “Song Moo Kwan Kong-Soo Do”. Alichukua yale aliyofundishwa na Funakoshi akaongeza mapokeo kutoka kwenye Tae Kyon na Soo Bakh Ki akatengeneza Song Moo. Kwahiyo si kwamba Song Moo Kwan ni Shotokan toka nitoke..hapana. Zinafanana baadhi ya misingi na kwamba zote zinatumia jina moja katika lugha mbili tofauti, sawa na kusema Musa na Moses au John na Yohana. Tofauti nyingine ni kwamba kutokana na mapokeo ya Taekyon kuwepo ndani ya Song Moo Kwan utaona kwamba ina miondoko inyofuata umbo la duara wakati Shotokan ni mtindo mnyofu. Hauna maduara.

Bahati mbaya maendeleo ya mfumo wake chini ya jina hili hayakuwa mazuri. Hii ilisababishwa na mambo makuu mawili:-

(i) Korea ndio imepata uhuru kwahiyo wakorea hawakupenda kujihusisha na ambacho kingewakumbusha utawala wa kikoloni wa wajapani. Pia kwa kuwa Song Moo Kwan ilikuwa ni tafsiri ya herufi za kijapani zinazotumika kuandika neno Shotokan utaifa uliingia na hivyo kufanya Song Moo Kwan kuonekana kana kwamba ni mapokeo ya utamaduni wa kijapani.

(ii) Korea kama taifa iliingia kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vilisababisha Korea kugawanyika kuwa Korea kusini na Korea kaskazini. Hali hii ilisababisha shule nyingi za sanaa za mapigano kufungwa huku walimu na wanafunzi wakiitwa jeshini.

Kutokana na hayo Kong-Soo Do ikafifia.

Mitindo mbalimbali iliyokuwa inaitwa Kong Soo ikatoweka au kubadilisha majina na kumezwa na mtindo mpya uliokuja kujulikana kama Tang-Soo Do.

Baadhi shule za mwanzo za Kong Soo Do ukiachia mbali Song Moo Kwan ni Chung Do Kwan, Chang Moo Kwan, Yun Moo Kwan, Ji Do Kwan nakadhalika.

Leo hii kuna shule chache mno zinazofundisha sanaa inayoitwa Kong-Soo Do.

Saturday, February 9, 2008

TAEKWON-DO

Taekwon-do ni sanaa ya mapambano ya kujilinda ya mikono mitupu ya asili ya Korea. Tofauti na watu wengi wanavyodhani, Taekwon-do kamwe siyo karate ya korea. Kwahiyo si sahihi kuiita sanaa hii kuwa ni karate ya korea. Karate ya Korea inaitwa Kong Soo Do ambayo ni tofauti kabisa na Taekwon-do.

Kwa bahati mbaya ufahamu wa watu wengi kuhusiana na sanaa za mapambano, (martial arts kwa lugha ya kiingereza) una misingi katika filamu. Kwenye miaka ya sabini filamu nyingi zenye kuonyesha mapambano ya aina hii zilijipatia umaarufu mkubwa sana. Jambo la kusikitisha ni kwamba watu wengi walichukulia kwamba mapigano yanayoonyeshwa kwenye filamu hizo ndio hayo yatumikayo katika hali ya kawaida, jambo ambalo si kweli kabisa. Vivyo hivyo Taekwon-do pia kama sanaa nyingine kutambulika kwake kulitokana na filamu na mashindano ya olimpiki. Hiyo ikapelekea watu wafikiri kuwa Taekwon-do ni sanaa ya mapambano ya michezo tu. Hii ni pamoja na baadhi ya walimu wa sanaa nyingine ambao wababaishaji, waliojipachika vyeo na kujiita wataalamu, wakati lengo lao ni kujipatia utajiri wa haraka kwa kudanganya watanzania wenzao na vile vile kukesha kila siku kugombea madaraka katika vyama vyao husika vya michezo badala ya kujali maendeleo ya elimu, kiwango na ufahamu wa wanamichezo wao kuhusu sanaa wanazozisimamia.

Kwanza kabisa ni lazima uelewe kuwa Taekwon-do ni tofauti na Karate, Judo, Muy Thai nakadhalika. Zote ni sanaa za mapambano lakini kuna tofauti kubwa.Mtu akichezea mpira haina maana kuwa anacheza soka, mpira wa kikapu au mpira wa mikono. Hiyo iliyotajwa hapo ni aina ya michezo ya mpira lakini yote ni tofauti katika namna ya kucheza kama vile zilivyo sanaa za mapambano.

Pili, walimu wengi wababaishaji huwadanganya watu kuwa Taekwon-do ni sanaa pekee ya mapambano ya mikono mitupu itokayo Korea. Hii si sahihi, kwani kuna sanaa nyingine nyingi zenye asili ya Korea achilia mbali Taekwon-do. Baadhi ni Kong Soo Do, Tang Soo Do, Hap Ki Do, Kuk Sool Won (inatamkwa kyuk suul wuon), Bulkyo Moo Sool, Kong Jong Moo Sool, Hoi Jeon Moo Sool, Hankido, Kumdo, Yudo na nyinginezo nyingi. Tutakuwa tunawaletea historia fupi za sanaa nyinginezo mbalimbali za Korea ili watu wapate ELIMU. Hii itajumuisha na historia ya miamba na waasisi mbalimbali wa sanaa hizo.

Tatu, wengi hudhani kuwa Taekwon-do hutegemea matumizi ya miguu tu yaani mateke katika mapambano. Ingawa kuna ukweli kidogo kuhusiana na matumizi ya miguu kwa sababu ni jambo linalofahamika kote duniani kuwa Taekwon-do ni maarufu kwa upigaji wa mateke mbali mbali lakini si kweli kuwa mateke ndio silaha pekee ya Taekwon-do. La hasha. Kuna silaha nyingi ndani ya Taekwon-do ikiwa ni pamoja na ngumi, vidole, mapigo ya mkono wazi, mapigo ya kuvunja mifupa, mapigo maalum ya kushambulia mishipa ya fahamu, umahiri wa kusokota na kuvunja mifupa na kutegua viungo, nakadhalika. Siri iliyopo hapa ni kwamba; mpiganaji wa Taekwon-do anapopewa nafasi ya kuchagua ni silaha ipi atakayokuwa tayari kuitumia kwa haraka katika pambano, basi yeye mara nyingi atachagua miguu, yaani teke. Ndio hii inapelekea watu kufikiri kuwa wapinaji wa sanaa hii wao hutumia mateke tu kwenye mapambano.

Duniani kuna vyama vikuu viwili vinavyosimamia Taekwon-do. Kuna International Taekwon-do Federation (I.T.F) na World Taekwondo Federation (W.T.F). W.T.F ndio inayo simamia Taekwon-do inayoshiriki kwenye olimpiki na I.T.F inasimamia Taekwon-do iliyoegemea kwenye mchepuo wa kujilinda ambayo hapo awali mwanzilishi na mwasisi wa Taekwon-do hiyo alikuwa ameitengeneza iwe maalum kwa ajili ya mahitaji ya wanajeshi vitani. Huyu naye alikuwa ni mwanajeshi mwenye cheo cha jenerali na aliitwa Choi Hong Hi. Sasa hivi ni marahemu. Aina hii ya Taekwon-do ni ya hatari sana kwahiyo huwa si vizuri kwa raia wasio wema kufundishwa na ndio maana inasisitiza nidhamu ya hali ya juu kama ile inayopatikana ndani ya jeshi. Kwa bahati nzuri hapa Tanzania aina hizi mbili zinapatikana.

Kuna habari zinazodai kuwa baadhi ya wadau wa sanaa hizi za mapambano ya mikono mitupu wanajenga hali ya ukaribu na ndugu zetu wa W.T.F. Si unajua kuwa mwaka huu kuna mashindano ya Olimpiki...So jamaa wanailia “taimingi” trip ya kwenda Beijing, China. Sasa sijui huko wanataka waende kama wachezaji au wasindikizaji. Sabum Prosper Makonya wa Arusha unazo hizi taarifa? Ni kweli?

Utaalamu wa kumvunja adui mfupa wa kiganja na kuvuruga mzunguko wake wa damu iendayo kwenye ubongo. Amiri salim (kushoto) na Simon msakanya (kulia) wote kutoka Tazania I.T.F. Taekwo-do.

Adui kulia!! Kihaap..Kumaliza pambano kwa pigo moja. Simon msakanya(kulia) akimpiga "adui" Amiri Salim(kushoto) pigo liitwalo "Sonkal Yop Taerigi". Jamaa ana uwezo wa kuvunja vigae vitano vilivyofungwa pamoja na kuwa furushi moja kwa pigo hilo. Swali..Je shingo yako kwa mbele hapa..usawa wa koromeo ni pagumu kuliko vigae vitano vilivyofungwa pamoja na kuwa furushi moja?

Maximillian Kailangana (Kulia), mdau wa Tanzania I.T.F. Taekwon-d0 akiwa na mheshimiwa mkuu wa wilaya ya ilala wakati wa uzinduzi wa Shirikisho la Wasanii Tanzania (SHIWATA). "Masela" msije mkambipu mheshimiwa..huyo mshikaji hapo atakung'oeni pua!!

Taekwon-do Crew..Baada ya Baptism by 200 squat jumps..yaani jozi mia mbili za "uchura mrefu". Kati ya watu kumi na tisa walibaki kumi!! Aminia baba 'ake..